KONGAMANO LA WADAU WA MICHEZO KUELEKEA CHAN NA AFCON
service image
15 Jan, 2025

Kamisheni Mtendaji wa kituo cha Ubia baina ya Sekta ya umma na sekta binafsi (PPPC) David Kafulila amewaita wawekezaji kuchangamkia fursa ya kuwekeza kwenye maeneo mbalimbali ya huduma za kijamii kuelekea mashindano ya chan na Afcon.

Rai hiyo imetolewa leo Januari 15 2025 katika hafla ya  kongamano  la wadau wa Michezo  kuelekea CHAN 2024 na AFCON 2027.

Amesema kuwa  wahakikishe wanaleta maandiko ya ubia ili kituo cha  cha ubia baina ya  sekta ya umma na binafsi kiweze kuyafanyia kazi.

“Wawekezaji  hii ni fursa ya kutoa huduma  hususani  katika mashindano hayo,” amesema.