Kuhusu BMT

 

Baraza la Michezo la Taifa (BMT) ni Taasisi ya Serikali yenye dhamana ya kusimamia sekta ya michezo nchini lililoundwa kwa mujibu wa sheria namba 12 ya mwaka 1967 sura ya 49, na kuanza rasmi mnamo tarehe 28 Aprili 1967.

 

 Majukumu BMT

  1. Kuendeleza, kustawisha na kudhibiti aina zote za Michezo kitaifa kwa ushirikiano na vyama au vikundi vya michezo.
  2. Kuhimiza na kutoa fursa za ushirikiano miongoni mwa vyama mbalimbali vya Taifa.
  3. Kuidhinisha mashindano ya kitaifa na ya kimataifa katika michezo na matamasha yaliyoandaliwa na vyama vya kitaifa na vyama vingine.
  4. Kupanga kwa kushirikiana na serikali za mitaa kwa ajili ya kutenga maeneo kwa ajili ya michezo.
  5. Kuhamasisha ushiriki wa jamii katika michezo.
  6. Kupanga na kuishauri Wizara yenye dhamana ya Michezo juu ya Sera ya ukuzaji michezo nchini.

 

 Aidha Baraza la Michezo la Taifa lina wajibu wa;

  1. Kuendeleza, kustawisha na kudhibiti aina zote za michezo ya ridhaa kwa kushirikiana na Vyama vya Michezo
  2. Kuhimiza na kutoa fursa na ushirikiano miongoni mwa Vyama vya michezo
  3. Kuidhinisha mashindano ya kitaifa na kimataifa ya michezo na matamasha yanayoandaliwa na Vyama vya michezo. 
  4. Kuandaa baada ya kushauriana na Vyama vya michezo vinavyohusika mashindano ya kitaifa na kimataifa nia ikiwa ni kubadilishana uzoefu na kukuza mahusiano ya kirafiki na mataifa mengine. 
  5. Kuamsha ari ya kupenda aina zote za michezo kwa ngazi zote.
  6. Kutoa baada ya kushauriana na vyama vya Taifa, Nishani, stashahada, vyeti,vikombe na vivutio vingine kwa ajili ya kuhimiza na kukuza shughuli za michezo
  7. Kudhamini nafasi za masomo kwa ajili ya mafunzo ya walimu wa michezo na waandaaji
  8. Kumshauri Waziri kuhusu mahusiano ya nje katika uwanda wa Michezo.
  9. Kushirikiana na mamlaka za serikali za mitaa ili kuwezesha kuwepo kwa fursa za michezo kwa ngazi zote na kujatahidi kujenga moyo wa uanamichezo na nidhamu kwa wanamichezo wote
  10. Kushauriana na vyama, taasisi au watu wengine kuhusiana na michezo ya ridhaa.

 

 Dira na Dhima

 DIRA

Kuwa na Taifa lenye watu wenye Afya, wakakamavu na ufanisi kwenye michezo kwa maendeleo ya jamii, umoja na taifa​​​​​​​

 DHIMA

Kutoa fursa sawa ya ushiriki kwa watu wote katika michezo ili kuongeza ufanisi”