KUFUZU OLIMPIKI: CHANGALAWE APOTEZA KWA POINTI DHIDI YA MNORWAY
service image
09 Mar, 2024

Jana ilikua siku mbaya kazini kwa bondia tegemeo wa Taifa Yusuf Changalawe baada ya kupoteza kwa maamuzi ya kutofautisha *(Split decision)* ambapo majaji 3 dhidi ya 2 walimpa ushindi mpinzani wake Mindaugas Gedminas kutoka nchini Norway.

Kwa matokeo hayo ya kupoteza kwa pointi 3-2 ni rasmi Changalawe amehitimisha safari yake katika mashindano haya ya kwanza ya Dunia ya kufuzu kushiriki Olimpiki ya Paris 2024. Alikua amebakisha mapambano 2 kushinda ili aweze kufuzu.

Changalawe anatarajiwa kuondoka Milano, Italy wakati wowote kuelekea Accra, Ghana kuungana na wenzake 7 kushiriki mashindano ya Afrika Accra 2023 ambapo ngumi zitaanza rasmi kupiganwa tarehe 14-03-2024.