UCHAGUZI TAWF

27 Oct, 2022
Majina ya wasailiwa waliopitishwa katika usaili wa wagombea wa nafasi tofauti za uongozi katika shirikisho la mieleka Tanzania (TAWF) uliofanyika leo Oktoba 27, 2022 katika ukumbi wa Uwanja wa Benjamin Jijini Dar es salaam.
Aidha, uchaguzi wa viongozi wa shirikisho hilo utafanyika kesho tarehe 28 Oktoba kuanzia saa 3 asubuhi katika ukumbi wa Msasani beach Club.