HAFLA ZA KUTUNUKIWA MEDALI KUFANYIKA LEO.
service image
07 Aug, 2022

Hafla za kutunukiwa medali kwenye mchezo wa ngumi katika kila uzani zitafanyika siku ya leo wakati wa mapambano ya fainali.

Tanzania 🇹🇿 itapata rasmi *medali mbili (2)* leo kupitia Mabondia wake wawili *Kassim Mbundwike* aka "Mfupa wa Sokwe" na *Yusuf Changalawe.*

Hafla ya kwanza kwa Tanzania itakua majira ya Uingereza saa 6:45 mchana *(Tanzania 8:45 mchana)* katika uzani wa Light heavyweight 75kg - 80kg ambapo *CHANGALAWE* atatunukiwa medali ya *SHABA* 🥉 (Bronze)

Hafla ya pili kwa Tanzania itafanyika majira ya Uingereza saa 10:30 jioni *(Tanzania saa 12:30 jioni)* katika uzani wa Light middleweight 67kg - 71kg ambapo Bondia *MBUNDWIKE* atatunukiwa medali ya *SHABA* 🥉(Bronze)

Mpaka kufikia sasa nchi ya *TANZANIA* imefanikiwa kushinda medali tatu (3), ambapo mbili (2) za Shaba 🥉 zimetokana na mchezo wa Ngumi na medali moja (1) ya fedha 🥈 ambayo imetokana na mchezo wa riadha kupitia kwa *Felix Simbu.*

Mara ya mwisho nchi yetu kupata medali katika michezo hii ya Jumuiya ya madola ilikua ni *miaka 16* iliyopita katika michezo ya *Melbourne 2006 (Dhahabu 1 na Shaba 1)* na kurudi mikono mitupu New Delhi 2010, Glasgow 2014 na Gold Coast 2018.