MALIASILI WAMPA UBALOZI WA UTALII WA HIARI RIO FERDINAND
service image
21 May, 2026

Waziri wa Maliasili na Utalii  Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ametangaza kumpa Ubalozi wa hiari wa Utalii wa Tanzania  Mchezaji wa zamani wa Klabu ya  Manchester United na  Timu ya Taifa ya Uingereza Rio Ferdinand.

Ubalozi huo umetangazwa tarehe 21 Mei, 2026 jijini Arusha, ambapo Mhe. Dkt. Ashatu ameeleza kuwa sekta ya utalii  inaingiza kiasi cha sh Bil.4.4 kwa mwaka.

"Rio ana wafuasi katika mitandao ya kijamii, ambapo yeye kuitaja Tanzania kufuatia  ziara aliyoifanya atawashawishi wafuasi hao kuja kutalii hapa Tanzania" amesisitiza Mhe. Ashatu.

Dkt. Ashatu ameongeza kuwa, hatua  hiyo ni mojawawapo ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ambayo imeelekeza kufikia watalii milionii 8 kwa mwaka mmoja.

Aidha, amempongeza Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kumleta mchezaji huyo nchini, ambapo ni njia mojawapo ya kutangaza nchi na vivutio vyake kimataifa.

Kwa upande wake mchezaji Rio ameshukuru ukarimu na hesehima aliyoipata, akiahidi kuitangaza Tanzania na kurudi tena kutembea.

slot gacor