MASHINDANO YA KANDA YA TANO MPIRA WA KIKAPU
![service image](https://www.bmt.go.tz/uploads/news/76e560f784d4dc988bb8eaa66512fa55.jpeg)
18 Jun, 2023
Timu ya taifa ya mpira kikapu wanaume (Tanzanite) imeanza vyema katika mashindano ya kanda ya tano yaliyofanyika jana juni 17 , 2023 kwenye uwanja wa ndani wa Benjamin Mkapa Dar es salaam.
Tanzania iliiibuka na ushindi wa vikapu 69-34 dhidi ya Eritrea katika mchezo uliopigwa kwenye uwanja ndani.
Mashindano hayo yameshirikisha nchi 10 na lengo ni kutafuta timu zitazofuzu kucheza mashindano ya Afrika.